"Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuboresha mazingira ya kufanya biashara kwa wajasiriamali wadogo (Machinga, Mama lishe, Baba lishe na Waendesha bodaboda, bajaji na maguta)".
Dkt. Samia Suluhu Hassan
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametanabaisha kuwa wamachinga ni watu muhimu katika kukuza pato la Taifa na takwimu zinaonesha kuwa sekta ya viwanda vidogo na biashara ndogo imetengeneza ajira, kukuza uchumi na kuondoa umasikini. Aidha, amesisitiza kwamba wamachinga ni watu muhimu sana na wamekuwa suluhisho la mahitaji kwa watu wengi kuanzia wenye kipato cha chini, kati na kipato cha juu, hivyo ametoa rai kwa Watanzania wote kuendelea kuunga mkono shughuli zao kwa vitendo.
Serikali imeziagiza mamlaka zinazohusika na ujenzi wa masoko mazuri unaoendelea kwenye maeneo mbalimbali nchini wazingatie na waandae miundombinu kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga.
Sekta hiyo ina jumla ya wajasiriamali milioni 3.1 ambao wameajiriwa ni asilimia 23.4 ya nguvu kazi ya Taifa na imechangia asilimia 27 katika pato la Taifa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan ameahidi kutoa shilingi milioni 10 kwa ajili kutatua
changamoto ya uendeshaji wa ofisi za Machinga mikoani.
Ahadi hiyo aliitoa alipozungumza kwa njia ya simu na Viongozi wa
Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) Mei 06, 2022 kupitia kwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima wakati wa mkutano wa mafunzo kwa viongozi wa Shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (Shiuma) kutoka mikoa yote Tanzania uliofanyika Jijini Dodoma.
Rais Dkt. Samia alibainisha kuwa, fedha hizo zitaanza kutolewa katika mwaka wa
fedha ulioanza mwezi Julai, 2022.
Sambamba na hilo, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wakuu wa mikoa nchini kuwapanga wamachinga katika maeneo stahiki bila kusababisha vurugu.
Dkt. Samia amesema licha ya serikali kutoa fursa kufanya biashara kama njia ya ajira kwao, ni lazima Serikali iwatengenezee mazingira rafiki nasio kufanya biashara kiholela kwenye maeneo yasiyo na usalama na utulivu kwao na mali zao.
Mfano wa masoko maalumu ya wamachinga yaliyojengwa kufuatia agizo la Rais Dkt. Samia ni Ujenzi wa
soko la wazi la Machinga lau Jijijni Dodoma ambao umegharimu kiasi cha
shilingi bilioni 9.53 mpaka kukamilika kwake ambapo
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa shilingi bilioni tatu
na Halmashauri ya Jiji ilitoa kiasi cha shilingi bilioni
sita na nusu kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.
Aidha, Rais Dkt. Samia wakati akizungumza na jamii ya wafanyabiashara ndogondogo (Wamachinga) alipowaalika Ikulu ya Dar Es Salaam, Rais Dkt. Samia alisema Serikali
yake imeshaanza kulifanyia kazi suala la kuyaboresha mazingira wafanyiayo kazi machinga kwa kutenga fedha
kwa ajili ya kuboresha baadhi ya masoko, ikiwemo
la Karikakoo.
Alitanabaisha kuwa ujenzi wake ukikamilika litakuwa na
uwezo wa kuchukua wafanyabiashara zaidi ya 4,000
ikilinganishwa na idadi ya 2,500 iliyokuwepo awali.
Rais Dkt. Samia amesema, Serikali inaendelea kutafuta
maeneo ya wazi, kwa ajili ya kujenga masoko katika
maeneo ya pembezoni mwa Miji, ili kuondoa
msongamano wa wateja katika masoko
yaliyokuwepo katikati ya Miji.